Barcelona, Real Madrid zapeta la liga

Barcelona wakicheza katika uwanja wao wa Nou Camp wamewachapa Sevilla kwa mabao 3-0, magoli ya Barca yakifunga na Luis Suarez na lionel Messi aliyefunga mara mbili.
Real Madrid wakiwa ugenini wameshinda kwa mabao 4-2 dhidi ya Leganes,Mshambuliaji Alvaro Morata akifunga hattrick na bao jingine likifungwa na James Rodriguez, mabao ya Leganes yakifungwa Gabriel Pires,na Luciano Neves.

Alaves wakalala nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Osasuna, Deportivo La Coruna wakatoshana nguvu na Granada kwa sare ya bila kufungana , Malaga wakawatambia Sporting Gijon nyumbani kwa kuwafunga bao 1-0.
Comments
Post a Comment